Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania, Hebron Mwakagenda.
JUKWAA
la Katiba Tanzania (Jukata), limemtaka Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la
Katiba Samuel Sitta kufuata sheria na kaanuni za bunge hilo.Akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Kaimu
Mwenyekiti wa Jukata, Hebron Mwakagenda alisema kuwa kwa sasa Sitta
hana mamlaka ya kukusanya maoni kwani ni kinyume na sheria ya tume ya
mabadiliko katiba.
“Tumeshuhudia
bunge maalumu la katiba likiongozwa na mheshimiwa Sitta likiendelea
kupokea maoni ya makundi mbalimbali wakiwemo wafugaji, waandishi wa
habari na wasanii ambapo ni kinyume na sheria,” alisema.
Mwakagenda
alifafanua kuwa hatua hiyo imekwenda kinyume cha sheria namba 9 (1)
ambacho kinaeleza kazi za tume ya mabadiliko ya katiba ambayo ilikuwa na
kazi ya kukusanya, kuchambua, kuandika taarifa na kuwasilisha kwenye
bunge ambapo kazi yake ni kuipitisha kama ilivyo kwenye kifungu cha
sheria namba 25.
Katika
suala la uondoaji wa vifungu kwenye rasimu hiyo alisema rasimu
imezingatia kero na malalamiko ya wananchi hivyo kuyaondoa ukilinganisha
na mantiki inayoendelea bungeni ni sawa na kurekebisha katiba ya mwaka
1977 na kubaki na malalamiko kwa wananchi kuwa viongozi hawawajibiki.
Pia
aliyataka makundi yanayopingana kwenda kwenyekikao kinachotarajiwa
kufanyika Ikulu wiki hii kwa moyo mkunjufu na kwa kuzingatia maslahi ya
taifa na si vyama vyao.
Hata
hivyo alisema kuwa pamoja na juhudi za kuendeleza mchakato wa katiba
mpya lakini mchakato huo hautokamilika na kutumika katika uchaguzi mkuu
wa mwaka 2015.
Alifafanua
kuwa hali hiyo imesababishwa na mwingiliano wa shughuli mbalimbali za
kiserikali zikiwemo za uandikishaji mpya wa vitambulisho vya kupigakura
katika mfumo mpya wa BVR.
Pia
alisema kuwa kupanda kwa joto la uchaguzi kwa sasa pia inaweza
kusababisha katiba kutopatikana kwani takribani wanasiasa wote
wamegeukia kwenye uchaguzi na si kupatikana kwa katiba.
“Sisi
kama Jukata tunashauri mchakato huu kuhairishwa hadi baada ya uchaguzi
mkuu na kuanza tena januari 2016 ili kuokoa gharama za uchaguzi kwa
kuunganisha na kufanyika chaguzi zote kwa mara moja,” alisema
Mwakagenda.
No comments:
Post a Comment