Friday, 29 August 2014

Huyu Mchezaji Wa Man United Ameteuliwa Kuwa Nahodha Wa Timu Ya Taifa Ya Uingereza

Mshambuliaji wa Man United Wayne Rooney ambaye hivi karibuni alipewa cheo cha kuwa Nahodha wa timu yake wa Man United sasa amekabithiwa cheo kingine kikubwa zaidi kwenye soka.
Baada ya Steven Gerrard kustaafu soka la kimataifa ,Rooney mwenye miaka 28 ameteuliwa kuwa nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza na kocha wake Roy Hodgson.Mpaka sasa Rooney amefunga magoli 40 kwenye mechi 95 na timu yake ya taifa. Kwenye website yake Rooney ameandika  “hii ni kazi nitakayojituma kuifanya kuliko,na nimefurahia sana uteuzi huu, ni kama ndoto kuwa kweli ”

No comments:

Post a Comment